Breaking

Friday 25 November 2022

AHUKUMIWA MIAKA 15 JELA KWA KUMKATA MUWEWE SEHEMU ZA SIRI




Esther Kaio wa Igembe Kasakazini, Kaunti ya Merua mempatwa na hatia ya kujaribu kumuua mumewe, kwa kumnyofoa sehemu zake nyeti.

Kwa mujibu wa ripoti ya Nation, Hakimu mkuu wa Maua Tito Gesora alimhukumu Esther kifungo cha miaka 15 jela baada ya kumvamia mumewe mnamo Novemba 19, 2021.

Wakati akijitetea, mama huyo wa watoto watano alidai kwamba alikuwa na matatizo ya kiakili, na hivyo hakumshambulia mumewe kimakusudi.

Esther aliishangaza mahakama baada ya kudai alijikuta amezuliwa na polisi, pasi na kujua makosa aliyokuwa amefanya.

Akitoa ushahidi wake, mwanamume huyo alikumbuka jinsi mkewe alivyomshambulia kwa panga saa tisa usiku kabla ya kuchukua kisu na kukata sehemu zake nyeti.

Mkulima huyo wa miraa wa miaka 60 alipatikana amezirai, huku mwanamke huyo akijaribu kumwekea kemikali mdomoni mwake.

Mahakama iliambiwa kwamba binti yake alisikia mfarakano na kuanza kupiga kamsa, ndipo majirani wakaja kumnsuru na kumpeleka babake katika Hospitali ya Misheni ya Chaaria.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages