Breaking

Friday 17 June 2022

WATU 1500 AFRIKA WAAMBUKIZWA MONKEYPOX, 66 WAFARIKI




Bara la Afrika limeripotiwa kuwa na Maambukizi 1,597 ya Virusi vya homa ya Nyani (MonkeyPox) tangu kuanza kwa mwaka 2022, hku Watu 66 wakiwa wamefariki dunia.


Akizungumza katika mkutano wa kila wiki na Vituo vya Afrika vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa jana Alhamisi Juni 16, 2022 Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa (CDC) Afrika, Ahmed Ogwell Ouma amesema Ugonjwa huo bado haujadhibitiwa katika bara la Afrika na kuongeza kuwa kampeni ya chanzo ya ugonjwa huo inapaswa kuanza barani Afrika.


"Msimamo wetu ni kwamba chanjo ni nyenzo muhimu na inahitaji kuanzia hapa Afrika, Hapa ... mzigo ni mkubwa, hatari ya juu na kuenea kwa kijiografia pia ni pana," amesema Ouma.


Nchi za Afrika ambazo zimeripoti kesi zilizothibitishwa ni Cameroon, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Nigeria, Morocco, Ghana, Liberia na Sierra Leone, Ouma alisema.


Shirika la Afya Ulimwenguni linatazamiwa kuitisha kamati ya dharura wiki ijayo kutathmini kama mlipuko wa tumbili unawakilisha dharura ya afya ya umma ya wasiwasi wa kimataifa.


Monkeypox ni ugonjwa wa kawaida katika sehemu fulani za Afrika. Zaidi ya nchi 30 ambapo ugonjwa wa virusi hauenea sana zimeripoti milipuko mwaka huu, nyingi zikiwa Ulaya.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages