Breaking

Monday 5 September 2022

BREAKING: MAHAKAMA YATHIBITISHA USHINDI WA WILLIAM RUTO URAIS KENYA




Mahakama ya juu imeidhinisha Uchaguzi wa William Ruto kuwa rais mteule wa Kenya baada ya kesi iliowasilishwa na mpinzani wake mkuu katika uchaguzi huo Raila Odinga kukosa ushahidi wa kutosha.


Wakitoa uamuzi wao wa pamoja, majaji hao walioongozwa na jaji mkuu Martha Koome walisema kwamba ushahidi uliotolewa na mlalamishi Raila Odinga ulikuwa umejaa uvumi na porojo.


Akiangazia maswala tisa ya kesi hiyo, Jaji Martha Koome amesema kuwa mshindi wa uchaguzi huo William Ruto alifanikiwa kupita kikwazo cha kura asilimia 50 na moja ya kikatiba.


Akitangaza matokeo hayo , mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) Wafula Chebukati, alimtangaza Dkt Ruto kuwa Rais mteule baada ya kupata kura milioni 7,176,141 (asilimia 50.49) dhidi ya milioni 6,942,930 za Bw Odinga (asilimia 48.85) )Prof George Wajackoyah wa Roots Party alifanikiwa kura 61,969 (asilimia 0.44) huku David Mwaure Waihiga wa Agano Party akiibuka wa nne kwa kura 31,987 (asilimia 0.23).


lakini akitoa uamuzi huo jaji mkuu Martha Koome alisema kwamba kura zilizokataliwa haziwezi kujumlishwa katika hesabu ya kumtafuta aliyeibuka mshindi.


Bi Koome alisema kwamba mbinu iliotumika na tume ya uchaguzi kupata asilimia 64.4 ya wapiga kura ilikuwa sahihi.

Chanzo: BBC

Martha Koome anasema waliowasilisha maombi hawakuwasilisha ushahidi wowote wa kuaminika wa udukuzi wa mifumo ya IEBC; inaongeza ripoti ya uchunguzi pia haikufichua ukiukaji wowote.

"Mahakama hii iliamuru kuchunguzwa kwa fomu 41 (34A) zilizoainishwa. Hakukuwa na tofauti kubwa zilizopatikana kati ya fomu zilizopakiwa kwenye tovuti ya IEBC na fomu zilizowasilishwa kwa Bomas. Hakuna ushahidi wa kuaminika uliotolewa kuonyesha fomu zilizotolewa kwa mawakala zilikuwa tofauti"

"Iwapo kulikuwa na usumbufu wa upakiaji na usambazaji wa Fomu 34A kutoka vituo vya kupigia kura hadi IEBC Public Portal. Mahakama ya Juu haipati ushahidi wa kuaminika kuthibitisha kwamba mtu yeyote alifikia, aliingilia au kubadilisha fomu za matokeo ya wapiga kura."

Aidha amewaonya mawakili dhidi ya kutoa ushahidi wa uongo; inataja hati ya kiapo ya John Githongo kuwa inaweza kuwa na uwongo.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages