Breaking

Saturday 8 October 2022

TUME YA MADINI YAIBUKA MSHINDI WA TATU MAONESHO YA MADINI GEITA



Tume ya Madini leo Oktoba 08, 2022 imeibuka mshindi wa tatu kwenye Kundi la Taasisi Wezeshi za Serikali katika Sekta ya Madini kwenye Maonesho ya Tano ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayoendelea katika Viwanja vya Bombambili mjini Geita.

Kikombe cha ushindi kimekabidhiwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Ashatu Kijaji aliyekuwa mgeni rasmi kwenye ufungaji wa maonesho hayo.

Ili kuendelea kutoa huduma zaidi kwa wananchi wa mkoa wa Geita na mikoa ya jirani, zimeongezwa siku mbili za maonesho hayo.



Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages