Breaking

Monday 6 February 2023

VIFO VYAFIKIA 1900 TETEMEKO LA ARDHI UTURUKI, SYRIA



Takriban watu 1,900 wanaaminika kufariki baada ya matetemeko mawili ya ardhi kupiga Uturuki na Syria.

Idadi ya waliothibitishwa kufariki kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea asubuhi ya leo nchini Uturuki sasa imefikia 1,121, mkuu wa Mamlaka ya kudhibiti Maafa na Dharura nchini humo amesema.



Idadi ya waliouawa nchini Syria sasa imefikia 783, kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, ambalo limekuwa likijumuisha takwimu kutoka kwenye mamlaka katika maeneo yanayoshikiliwa na serikali na wale wa kundi la uokoaji la The White Helmets katika maeneo yanayodhibitiwa na waasi.

Takwimu zinaleta jumla ya pamoja kuwa takribabi 1,797.



Taarifa bado zinaibuka kuhusu athari za tetemeko la pili lililokumba mkoa wa Kahramanmaras nchini Uturuki saa chache baada ya lile la kwanza kutokea karibu na mji wa Gaziantep, karibu maili 80 kusini.

Watu wapatao 70 walikuwa tayari wamethibitishwa kuuawa huko Kahramanmaras kabla ya tetemeko la pili kupiga.

Idadi ya waliofariki sasa inatarajiwa kuongezeka huku juhudi za kuwaokoa zikiendelea.


Via: BBC
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages