Breaking

Wednesday 17 May 2023

ISW YASHIRIKI MAONESHO YA NACTVET JIJINI ARUSHA

Chuo cha Ustawi wa Jamii kinashiriki katika maonesho ya vyuo vya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (NACTVET) yanayofanyika katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Karume Jijini Arusha kuanzia tarehe 16 Mei 2023 ambayo yatadumu mpaka tarehe 22 Mei 2023.

Katika maonesho hayo Chuo cha Ustawi wa Jamii kimepata fursa ya kuelezea kozi mbalimbali zinazotolewa na Chuo, kutoa huduma ya usajili wa wanafunzi pamoja na kutoa elimu, ushauri, na msaada wa kisaikolojia (bure) kwa watu mbalimbali waliotembelea katika banda la Chuo.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages