Breaking

Wednesday 30 August 2023

DAKTARI FEKI AKAMATWA MUHIMBILI AKITAPELI WAGONJWA



Hospitali ya Taifa Muhimbili imemkamata mkazi wa Mbagala mkoani Dar es Salaam aliyejitambulisha kwa jina la Mussa Mawa akijihusisha na utapeli kwa wananchi wanaopata huduma hospitalini hapo.

Mkuu wa Idara ya Ulinzi wa hospitali hiyo, Alfred Mwaluko amesema kuwa daktari huyo feki amebainika akiwa kwenye harakati za kuwatapeli wananchi wanaouguza ndugu yao aliyelazwa jengo la Mwaisela.

Kijana huyo anayekadiriwa kuwa na miaka 35- 40 amesema ana takribani siku sita akifanya utapeli hospitalini hapo, na kueleza kuwa vazi la kidaktari alilianua wakati likiwa limeanikwa baada ya kufuliwa, na kitambulisho alitengenezewa na kijana aliyekuwa akipita eneo hilo.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma, Aminiel Aligaesha ametoa rai kwa watu wote wanaojihusisha na kutapeli wananchi katika eneo la hospitali kuwa ulinzi umeimarishwa na wakijaribu kufanya hivyo watakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya usalama.




Via:ST
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages