Breaking

Wednesday 29 November 2023

DKT. YONAZI ARIDHISHWA MAANDALIZI KUELEKEA SIKU YA UKIMWI DUNIANI

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi ametembelea mabanda mbalimbali na kujionea maandalizi yaliofanywa na wadau mbalimbali kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani yatakayofanyika 1 Disemba,2023 katika Viwanja vya Morogoro Sekondari ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa(mb).

Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni "Jamii Iongoze Kutokomeza UKIMWI"

Aidha ametumia nafasi hiyo kuwahimiza wananchi kujitokeza katika maadhimisho hayo na kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI Nchini.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages