Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Magdalena K.Rwebangira leo tarehe 01 Mei, 2025 ametembelea na kukagua vituo vya kuandikishia wapiga Kura vilivyo katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga ikiwa ni siku ya kwanza ya kuanza kwa zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili, mzunguko wa kwanza na uwekaji wazi wa daftari unaojumuisha mikoa 15 nchini.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeanza Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya Pili, mzunguko wa kwanza na uwekaji wazi wa Daftari la awali kwa mikoa 15 nchini ikiwemo na mkoa wa Rukwa kuanzia tarehe 01 Mei, 2025 hadi tarehe 07 Mei, 2025 ambapo vituo vitafunguliwa kuanzia saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 Jioni.


