Breaking

Sunday 20 March 2022

AJINYONGA BAADA YA KUMJERUHI MUMEWE KWA PANGA



Na Mwandishi Wetu

Mwanamke mmoja Mkazi wa kitongoji Kijiji cha Sibwesa wilayani Tanganyika Mkoani Katavi, amejinyonga akihofia kupata kesi ya mauaji baada ya kumjeruhi mume wake kwa kumkata mapanga.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo leo Jumapili Machi 20, 2022 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, ACP Ally Makame amesema kuwa wanafamilia hao hawakuelewana wakati wa mazungumzo yao ambapo ilitokea sintofahamu ikapelekea ugomvi kutokea ndipo Mande Emanuel (30) aliamua kumkata na panga mumewe 
Dotto Enos (35) na kumjeruhi vibaya.

“Alipogundua mume wake anaweza kufa akahofia kupata kesi ya mauaji, alizunguka nyuma ya nyumba yao akapasua kitenge chake akajinyonga, mume alipelekewa hosptali ya rufaa mkoa kutibiwa,” amesema Kamanda Makame

Kamanda makame amesema kuwa chanzo cha tukio hilo ni ugomvi wa kifamilia uliosababishwa na shughuli za kilimo.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages