Breaking

Tuesday 26 April 2022

RAIS SAMIA ATOA MSAMAHA KWA WAFUNGWA 3,826




Katika kuadhimisha Miaka 58 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Rais Samia Suluhu Hassan amewasamehe wafungwa wapatao 3,826 kwa masharti mbalimbali.

Msamaha huo utahusisha Wafungwa wanaotumikia adhabu kwa makosa ya usafirishaji wa Dawa za Kulevya ambao wamekaa gerezani kuanzia miaka 20 na kuendelea

Aidha, pia utahusisha Wafungwa wanaotumikia adhabu kwa makosa ya wizi au ubadhirifu wa Fedha na Mali za Umma ambao wamekaa gerezani kuanzia miaka 15 na kuendelea







Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages