Breaking

Tuesday 26 April 2022

WANAUME WANAONYIMWA UNYUMBA WATAKIWA KURIPOTI POLISI




Wanaume wanaofanyiwa ukatili wa kijinsia ikiwamo kupigwa na kunyimwa unyumba na wake zao majumbani, wametakiwa kwenda Polisi kutoa taarifa juu ya unyanyasaji huo wa kibinadamu katika Dawati la Jinsia, ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria.

Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi Kata ya Malambo Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Leyla Mhando, akiwa kwenye Kikao na Viongozi wa Serikali za Mitaa, amewataka wanaume wanaokung'utwa na kunyimwa tendo la ndoa na wake zao kutokuogopa kwenda kuripoti Polisi, ili wahusika washughulikiwe kulingana na sheria za nchi.

Amesema ukatili wa kingono, vipigo, saikolojia na ule wa kiuchumi unapaswa kudhibitiwa kuanzia ngazi ya familia, vinginevyo vinaweza kusababisha vifo na ulemavu dhidi ya binadamu.



Source:Eatv

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages