Breaking

Tuesday 7 June 2022

SHAKA ATAKA WATUMISHI WA TRA MTWARA KUCHUNGUZWA





Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Mtwara na TAKUKURU kuhakikisha wanafuatilia na kuwachukulia hatua baadhi ya Watumishi wa Mamlaka ya Mapato (TRA) Mkoani humo ambao wamekuwa sio waadilifu na kuwanyanyasa Wafanyabiashara kwa kuwafungia biashara zao.

Shaka ameyasema hayo katika kikao cha majumuisho ya ziara yake ya siku nne Mkoani Mtwara.

"Mkuu wa Mkoa huko TRA kuna mambo inabidi mkayaangaliee, Rais alipoingia madarakani jambo moja kubwa alilolifanya ni kufungua uchumi wa nchi, kuna biashara zilifungiwa Rais alipoingia zikafunguliwa"

"Kuna Watu wanafungia Watu biashara lakini TAKUKURU tusaidieni mkitaka tuwasaidie tutawapa baadhi ya Watumishi wa TRA vitendo wanavyofanya haviendani na maadili ya kazi zao"

"Kumekuwa na wimbi la kufunga biashara za Watu kwa makosa madogomadogo ambayo hayana msingi hatuwezi kuona dhamira njema ya Rais inakwamishwa baadhi ya Watu wanataka kumkwamisha Rais Samia"
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages