Breaking

Monday 13 June 2022

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUSHIRIKIANA NA WADAU KUTANGAZA UTALII WA UTAMADUNI NA MALIKALE


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja amesema Wizara ya Maliasili na Utalii iko tayari kutoa ushirikiano kwa wadau wanaofanya jitihada za kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kuandaa matamasha ya kutangaza utalii wa utamaduni na malikale.


Mh. Mary ameyasema hayo leo Juni 13, 2022 ofisini kwake jijini Dodoma alipokutana na waandaaji wa tamasha la Nandete Majimaji Festival litakalofanyika kuanzia tarehe 13 mwezi Agosti 2022 na kumalizika 15 mwezi Agosti 2022 katika  Kata ya Kipatimo Kijiji cha Nandete Wilaya ya Kilwa.


Tamasha hilo lenye kauli mbiu ya “Majimaji Tujiandae Kuhesabiwa” litahusisha mashindano ya mbio, mashindano ya mpira wa miguu na mashindano ya ngoma za asili ambapo washindi watapewa zawadi mbalimbali.



Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages