Breaking

Friday 29 July 2022

WAZIRI MCHENGERWA, BALOZI MIGIRO WASHIRIKI UZINDUZI MASHINDANO YA JUMUIYA YA MADOLA



Na John Mapepele

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa usiku wa kuamkia leo Julai 29 ameshiriki uzinduzi rasmi wa mashindano ya Jumuiya ya Madola nchini Uingereza.

Ufunguzi huo wa mashindano ya mwaka huu yamefana huku wageni kutoka nchi mbalimbali duniani za Jumuiya ya Madola wakiwa wameshiriki.

Timu ya wanamichezo inayoshiriki mashindano haya kutoka Tanzania nayo iliingia katika uwanja wa michezo huku ikiwa na hamasa. nyingine na kushangiliwa na maelfu ya watazamaji.


Katika tukio hilo Mhe. Mchengerwa akiambatana na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Dkt, Asha Rose Migiro, Mhe. Musa Sima (Mb) na Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Huduma na Maendeleo ya Jamii na Naibu Katibu Mkuu. Saidi Yakubu alipata fursa ya kubadishana mawazo na viongozi kutoka nchi mbalimbali duniani kwenye maeneo ya sekta ya Michezo.

Mhe. Balozi Migiro amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Samia Suluhu Hassan kwa kuweka kipaombele kwenye michezo.

Mhe. Mchengerwa amesema kuwa Tanzania imejifunza mambo mengi kwenye mashindano haya ambapo amesisitiza kuwa baada ya kurejea nyumbani kutafanyika maboresho makubwa.

Aidha, amesema dhamira ya Serikali kwa sasa ni kuhakikisha kuwa michezo inaendelezwa ili kutoa ajira na kuchangia kwenye uchumi wa taifa.

Amesema kwa sasa Serikali inakwenda kutekeleza mkakati wa kusaka vipaji vya michezo wa mtaa kwa mtaa.

Naye Mhe.Sima amesema kuwa michezo iwe fursa ya kuimarisha diplomasia na nchi nyingine.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages