Breaking

Wednesday 20 July 2022

RAIS SAMIA ATEUA MKUU MPYA WA JESHI LA POLISI


Na Lango La Habari

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amempandisha cheo Kamishna wa Polisi Camillus Mongoso Wambura na Kumteua kuwa Inspekta Jenerali na Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP).

Kupita taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa mawasiliano ya Rais Ikulu Zuhura Yunus imeeleza kuwa Uteuzi huo umefanyika usiku wa kuamkia leo Alhamisi Julai 20, 2022 ambapo kabla ya kuteuliwa alikuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa makosa ya Jinai (CDI).

Pia Rais Samia amemteua aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Simon Sirro kuwa Balozi wa Tanzania Nchini Zimbabwe.

Wakati huo huo amempadisha cheo Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Ramadhan Hamis Kingai kuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa makosa ya Jinai (CDI).

Uteuzi mwingine ni kama ifuatavyo:









Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages