Breaking

Monday 22 August 2022

MAGU YATAFUTA MWAROBAINI CHANGAMOTO YA WAFUGAJI HIFADHI YA SAYAKA



Mkuu wa Wilaya ya Magu, Mhe. Salum Kali amekutana na viongozi wa Chama na Serikali wa Wilaya hiyo kujadili mikakati ya kutatua changamoto ya wafugaji katika Hifadhi ya Sayaka Wilaya ya Magu.

Kikao hicho kimefanyika leo katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Magu.

Mhe.Kali amesema moja ya mwarobaini wa tatizo hilo ni kujenga malambo ya kunyweshea mifugo ili kuzuia wananchi kuingiza mifugo hiyo hifadhini.

Naye, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhe Mary Masanja amesema suala la uvamizi wa hifadhi ya Sayaka linatakiwa kutatuliwa kwa kushirikisha Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages