Breaking

Monday 19 September 2022

WAVAMIZI HIFADHI YA MSITU WA BONDO WATAKIWA KUONDOKA



Wananchi waliovamia Hifadhi ya Msitu wa Bondo wametakiwa kuondoka ndani ya hifadhi hiyo ifikapo Desemba 30,2022.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kilindi Mhe. Omar Mohamed Kigua bungeni jijini Dodoma leo Septemba 19,2022.

“Kwa nyakati tofauti hifadhi hii imekuwa ikivamiwa kwa ajili ya shughuli za kibinadamu zikiwemo kilimo,makazi na kuchungia mifugo” Mhe. Masanja amefafanua.

Amesema Serikali imeweka matangazo ya kuwataka wananchi wote kuondoka ndani ya hifadhi hiyo.

Aidha, amesema Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya inaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa Uhifadhi na matumizi endelevu ya rasilimali misitu nchini.

Hifadhi ya Msitu wa Bondo, ipo katika Kijiji cha Mswaki,Kata ya Msanja Wilayani Kilindi Mkoani Tanga.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages