Breaking

Friday 2 December 2022

AJALI YAUA WATATU, YAJERUHI 18 - MWANZA




Watu watatu wamepoteza maisha na wengine 18 kujeruhiwa kwenye ajali iliyohusisha magari manne katika eneo la Nyakato Sokoni jijini Mwanza.

Chanzo cha ajali hiyo kinatajwa kuwa ni gari aina ya TATA lililokuwa limebeba matofali kufeli breki

Ajali hiyo imetokea leo Desemba 1/2022 saa mbili asubuhi ambapo inadaiwa loli hilo lilifeli breki na lilipofika kwenye taa za kuongozea magari katika eneo la Nyakato sokoni ndipo likagonga magari manne na kusababisha ajali hiyo iliyouwa watu watatu huku dereva akikimbia

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Wilbroad Mutafungwa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.


Via: EATV
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages