Breaking

Tuesday 27 December 2022

AMUUA MDOGO WAKE WA MIAKA 13 WAKIZOZANA ZAMU YA KUPIKA



Msiba umegubika familia moja katika kijiji cha Ikorongo, kata ya Miruka, Kaunti ya Nyamira, baada ya mvulana wa miaka 15 kumuua kakake kwa kuzozania jukumu la kupika.

Tukio hilo lilithibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Kaunti Ndogo ya Nyamira Kusini (SCPC) Moses Kirong’ baada ya naibu chifu wa kata ya Miruka Robert Maugo kupiga ripoti kuhusu tukio hilo.

Ripoti zinasema kwamba kaka hao wawili walikuwa na mdogo wao wakipika wali walioachiwa na bibi yao wale mchana wakati hakuwa.

Kwa mujibu wa Kenya News Agency, kila mmoja alikuwa na zamu ya kuangalia iwapo wali umeiva, ila kaka yao mdogo alikataa jukumu hilo na vita vikaibuka na kusababisha kifo.

“Wakati zamu ya mwendazake ilipowadia ya kuangalia wali uliokuwa jikoni, alikataa hadi kakae mkubwa akasisitiza ila hakukubali na kundelea kucheza na kaka yake mdogo wa miaka 7,” naibu chifu alisimulia.

Kirong’ alisema kulinaga na kakake mdogo aliyeshuhudia tukio hilo, mwendazake alipigwa kwenye kifua wakati wa fujo hizo na kupotza fahamu baada ya kugongwa ngumi kwenye mbavu.

Mkuu huyo wa polisi alisema hatimaye kaka hao wawili waligundua kwamba amezirai na, kaka mkubwa akajaribu kumfufua ila haikufua dafu, hata alipomwagia maji baridi mwilini mwake.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages