Breaking

Sunday 11 December 2022

BABA AMBAKA MWANAE WA MIAKA 6


Jeshi la Polisi wilayani Babati mkoani Manyara, linamshikilia Elias Hando (30) mkazi wa Kijiji cha Tsaayo, Kata ya Arri wilayani humo kwa tuhuma za kumbaka mwanae wa kumzaa mwenye umri wa miaka 6.

Awali mtoto huyo alifanyiwa ukatili wa kubakwa na mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Ami Matle, ambaye alifungwa jela miaka 30 ambapo safari hii tena Baba yake mzazi amekamatwa kwa tuhuma za kumbaka mwanae.

Polisi wamemshikilia wanaendelea na uchunguzi wao wakimaliza watamfikisha mahakamani.

Via: EATV
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages