Breaking

Monday 16 January 2023

AJALI YA GARI YAUA WATANO, YAJERUHI WANNE KILIMANJARO




Watu watano wamefariki dunia papo hapo baada ya lori lililobeba katoni za maji ya kunywa kufeli mfumo wa breki katika eneo la mteremko barabara ya Mwika-Himo na kuigonga kwa nyuma gari dogo la abiria aina ya Toyota Noah lililokuwa likitokea Rombo kwenda Moshi, Mkoa wa Kilimanjaro.

Ajali hiyo imetokea jioni Jumapili Januari 15, 2023.

Daktari wa hospitali ya Faraja, Samweli Minja amethibitisha kupokea miili ya watu watano na majeruhi wanne.


"Ni kweli tumepokea miili ya watu watano wako mochwari na majeruhi wanne leo hapa hospitalini kwetu," amesema Dk Samweli

Kamanda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza anaeleka eneo la tukio na atatoa taarifa baada ya kufika na kuona hali ilivyo

"Naelekea eneo la tukio kulikotokea ajali nikifika nitatoa taarifa kamili,"amesema Kamanda Maigwa


Chanzo - Mwananchi

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages