Breaking

Thursday 12 January 2023

AMUUA BIBI YAKE KWA KUCHOMA MOTO NYUMBA AKIWA NDANI KISA KUMYIMWA PESA



Wenyeji wa Kijiji cha Eshitimba, Kaunti ya Kakamega wametamaushwa na kifo cha ajuza wa miaka 89.

Floice Lisero, alikufa moto baada ya mjukuu wake wa kiume mwenye umri wa miaka 40, kuteketeza nyumba yake kufuatia mzozo kuhusu pesa.

Mshukiwa huyo tayari amekamatwa na polisi, na inadaiwa alimshambulia bibi yake baada ya kukataa kumpa pesa alizomuitisha.

Kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Khwisero Samuel Kogo alithibitisha mkasa huo, akisema kwamba polisi walimuokoa mshukiwa huyo kutoka kwa wanakijiji waliojaribu kumpiga kitutu katika soko la Ebukambuli.

Kamanda huyo alisema kwamba mwanamume huyo atapimwa akili kubainisha iwapo yuko sawa au tahira, kabla ya kufunguliwa mashtaka dhidi yake.

“Ni lazima tumpeleke akapimwe akili ili kuthibitisha iwapo ako timamu au la kabla ya kumfungulia mashtaka yoyote,” Kogo alisema.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages