Breaking

Thursday 12 January 2023

MWANACHUO AJINYONGA KISA KUKATALIWA NA MWANAMKE ALIYEMLIPIA KODI NA KUMNUNULIA IPHONE 14



Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Gunze Luhangija aliyekuwa akisomea Shahada ya Menejimenti ya Ushirika na Uhasibu (BCMA), amekutwa amejinyonga chanzo kikisemekana ni kutokana na msongo wa mawazo uliosababishwa na kukataliwa na mpenzi wake.

Inadaiwa alishawahi kujaribu kujiua kwa kunywa sumu Januari 4 mwaka huu lakini aliokolewa baada ya kukataliwa ilihali ikieleza kuwa alimgharamikia mpenzi wake huyo ikiwemo kumpangishia nyumba.

Baadhi ya wanafunzi kutoka chuoni hapo wamedai marehemu alikuwa na ugomvi na mpenzi wake siku chache baada ya kumnunulia simu janja aina ya iPhone 14 iliyopelekea kuwa katika hali ya msongo wa mawazo.

“Siku ya Boxing Day alimnunulia mpenzi wake iPhone 14 na baada ya siku chache demu (mpenzi) alimkataa kwamba kapata mtu mwingine [..] dogo kajitundika,” mmoja wa wanafunzi chuoni hapo.

Aidha, Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Yahya Mdogo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa jeshi linaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha kifo chake.


Via: Swahili Times
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages