Breaking

Wednesday 8 February 2023

ZOEZI LA UOKOAJI LAENDELEA, IDADI YA WALIOFARIKI YAFIKIA 9,000 TETEMEKO LA ARDHI UTURUKI, SYRIA



Zaidi ya watu 9,000 wanajulikana kuuawa nchini Uturuki na Syria kufuatia tetemeko la ardhi la Jumatatu. Idadi ya watu waliouawa nchini Uturuki imeongezeka hadi 6,957, kulingana na shirika la maafa nchini humo.

Ni vigumu kuthibitisha idadi hiyo nchini Syria, lakini vyombo vya habari vya serikali na kundi la uokoaji vinasema takriban watu 2,500 wamefariki..

Kadiri ukubwa wa maafa ulivyozidi kudhihirika zaidi, idadi ya waliofariki ilionekana uwezekano wa kuongezeka kwa kiasi kikubwa. Afisa mmoja wa Umoja wa Mataifa alisema huenda maelfu ya watoto wamefariki.



Rais wa Uturuki Tayyip Erdogan alitangaza hali ya hatari katika majimbo 10. Lakini wakaazi katika miji kadhaa iliyoharibiwa ya Uturuki walionyesha hasira na kukata tamaa kwa kile walichosema ni jibu la polepole na lisilotosha kutoka kwa mamlaka juu ya tetemeko baya zaidi kuwahi kuikumba Uturuki tangu 1999.

Erdogan alitangaza majimbo 10 ya Uturuki kuwa eneo la maafa na akaweka hali ya hatari kwa miezi mitatu ambayo itairuhusu serikali kupita bunge katika kutunga sheria mpya na kuweka kikomo au kusimamisha haki na uhuru.

Serikali itafungua hoteli katika kitovu cha utalii cha Antalya ili kuwahifadhi kwa muda watu walioathiriwa na tetemeko hilo, alisema Erdogan, ambaye anakabiliwa na uchaguzi wa kitaifa katika muda wa miezi mitatu.





Via: BBC
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages