Breaking

Sunday 19 November 2023

NYAMAHANGA AZINDUA RASMI MASHINDANO YA MUHALILA CUP

Mkuu wa wilaya ya Muleba Dkt Abel Nyamahanga akizungumza wakati akizindua rasmi  mashindano ya mpira wa  Miguu ya Muhalila Cup ambayo yanafanyika kata ya Kagoma wilaya ya Muleba mkoani Kagera.
Mkurugenzi na mwandaaji wa mashindano ya Muhalila Cup Bwana Fortunatus Muhalila


Na Mariam Kagenda _ Muleba

Mkuu wa Wilaya ya Muleba Dkt Abel Nyamahanga amezindua rasmi  mashindano ya mpira wa  Miguu ya Muhalila Cup ambayo yanafanyika kata ya Kagoma wilaya ya Muleba mkoani Kagera.

Akizungumza wakati akizindua mashindano hayo Dkt Nyamahanga amesema kuwa michezo inajenga umoja,inaleta upendo na kufahamiana kupitia michezo hivyo anaishukuru kamati ya maandalizi ya mashindano hayo.

Dkt. Nyamahanga amesema serikali haijaiacha nyuma  michezo kwani iko  katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi  hivyo wananchi wanatakiwa kushiriki kwa pamoja katika mashindano hayo.

Naye Mkurugenzi  na muandaaji wa mashindano hayo Bwana Fortunatus  Muhalila amesema lengo la mashindano hayo ni kuibua vipaji vya vijana kupitia mchezo wa mpira  ambapo mashindano hayo hufanyika mwezi Novemba kila mwaka.

Ameongeza kuwa tangu mashindano hayo yaanzishwe mwaka 2015 wapo vijana wengi ambao wameshafanikiwa kupitia mashindano ya Muhalila cup kwani yupo kijana mmoja ambaye anachezea timu ya Kagera Sugar alitokea katika mashindano hayo.

Amesema kuwa lengo lake kubwa  ni kuona vijana wenzake wenye vipaji wanatoka hapo walipo wanasonga mbele  na kuwapa fursa vijana kuonyesha vipaji vyao ili waweze kuonekana                   

Kwa upande wake mgeni maalum ambaye ni mtangazaji wa habari za michezo kutoka Cloud Tv   Shafii Dauda amesema kuwa  yeye kama mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya   Ndondo atahakikisha wanashirikiana na wadau wa michezo ili kuendeleza vipaji vya vijana kupitia michezo ili waweze kusonga mbele.

Wakati akisoma risala Bwana  Omary Rwakyaya amesema kuwa jumla ya timu 16 zitashiriki mashindano hayo ambayo yatahitimishwa mwishoni mwa mwezi Desemba na Mshindi  wa kwanza atapata zawadi ya shilingi milioni 2, mshindi wa pili milioni 1 na mshindi wa 3 laki 5.

Wakati wa  uzinduzi wa mashindano hayo Timu ya New Muleba Breaking News Fc  imeifunga bao mbili timu ya Muyenje .

Omary Rwakyaya akisoma risala
Wachezaji wa Timu ya New Muleba Breaking News
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages