Na Samir Salum
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetia saini Hati za Makubaliano (MoU) 36 wakati wa mkutano wa Biashara na Uwekezaji uliofanyika Dubai leo Febınıari 26, 2022.
Kupitia taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu Bi. Zuhura Yunus imesema kuwa Hati 12 kati ya hizo zimetiwa saini baina ya Serikali ya Tanzania kupitia wızara na taasisi za umma na wawekezaji mbalimbaIi wa sekta za umma na binafsİ.
Vile vile, hati za makubaliano nyingine 23 zimetıwa saini baina ya makampuni binafsi kutoka Tanzanİa na makampuni mengine yenye nia ya kushirikiana katika sekta mbalİmbaIİ za kiuchumİ.
Hati moja itahusisha Wizara ya Biashara na Viwanda ya Zanzibar na wawekezaji wanaonuia kushirikiana kwenye sekta ya utalii.
Akiongea katika mkutano huo wa Biashara na Uwekezaji, Rais Samia Suluhu Hassan amesema ili kushawishi uwekezaji na kutengeneza bidhaa madhubuti na za kisasa, nchi İnahitaji elimu bora.
"Leo naisihi hasa Serikali ya UAE na nchi nyingine zinazoshiriki kwenye Expo Dubai kutoa fursa kwa wanafunzi wa Tanzanİa kusoma kupitia ufadhili na mpango wa ubadilishaji wa wanafunzi.”
Idadi ya ajira zinazotarajiwa kupatikana kwa ujumla kutokana na makubaliano hayo ni zaidi ya 200,000 katika kipindi cha miaka minne, huku uwekezaji huo ukigharimu zaidi ya dola bilioni 7.49 ambayo ni sawa na shilingi trilioni 17.35 za Tanzanıa.
Sekta zinazotarajiwa kunufaika na hati hizo za makubaliano ni pamoja na nishati, kilimo, utalii, miundombinu, usafiri,teknolojia.
"Leo naisihi hasa Serikali ya UAE na nchi nyingine zinazoshiriki kwenye Expo Dubai kutoa fursa kwa wanafunzi wa Tanzanİa kusoma kupitia ufadhili na mpango wa ubadilishaji wa wanafunzi.”
Idadi ya ajira zinazotarajiwa kupatikana kwa ujumla kutokana na makubaliano hayo ni zaidi ya 200,000 katika kipindi cha miaka minne, huku uwekezaji huo ukigharimu zaidi ya dola bilioni 7.49 ambayo ni sawa na shilingi trilioni 17.35 za Tanzanıa.
Sekta zinazotarajiwa kunufaika na hati hizo za makubaliano ni pamoja na nishati, kilimo, utalii, miundombinu, usafiri,teknolojia.