Breaking

Saturday 5 March 2022

URUSI YATANGAZA KUSITISHA MAPIGANO KWA MASAA MATANO KURUHUSU RAIA KUONDOKA UKRAINE



Na Samir Salum 

Wizara ya ulinzi ya Urusi imetangaza kipindi kifupi cha usitishaji wa mapigano na kuwaruhusu kwa raia  kuondoka katika miji ya Mariupol na Volnovakh kusini-mashariki mwa ukraine.

Raia wataruhusiwa kuondoka katika mji wa Mariupol nchini Ukraine kati ya saa Sita mchana hadi saa 11 jioni (12 : 00-17 : 00 )  kwa saa za Moscow siku ya leo Jumamosi Machi 05, 2022.

Wizara ya ulinzi ya Uruzi imethibitisha hilo na mapema leo Jumamosi na kuongeza kuwa wanajeshi wake ambao wameuzingira mji wa bandari wa Bahari ya Azov kusini mwa Ukraine wataacha kufyatua risasi na kuruhusu raia kupita.

 "Kuanzia saa 10 : 00 asubuhi kwa saa za Moscow (07 : 00 GMT), upande wa Urusi unatangaza kusitisha mapigano na kufunguliwa kwa korido za kibinadamu ili kuruhusu raia kuondoka Mariupol na Volnovakha," mashirika ya habari ya Urusi yalinukuu wizara ya ulinzi ya Urusi ikisema.


Mariupol ni mji muhimu wa bandari na imekuwa ikikabiliwa na mashambulizi kutoka Urusi kwa siku kadhaa. 

Kumekuwa na mapigano makali Volnovakha
Mapema, meya wa Mariupol alitoa wito wa raia kuruhusiwa kuondoka huku kukiwa na kile alichokiita "kizuwizi" cha vikosi vya Urusi

Wakati huo huo, Wizara ya Ulinzi ya Ukraine leo Jumamosi imesema kuwa zaidi ya wanaume 66,200 wa Ukraine wamerejea kutoka nje ya nchi kupigana.

Kwingineko, mapigano yanaendela. Milipuko mingi ilisikika katika Kharkiv, Kaskazini Mashariki mwa ukraine

Katika mji wa mashariki wa Sumy ambao umezingirwa na vikosi vya Urusi mashambulio ya anga yalianzakumi na moja alfajiri, kulingana na vyombo vya Habari vya Ukraine.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages