.jpeg)
Akithibitisha kukamatwa kwa watu hao Kamanda wa Polisi kanda Maalum ya Dar es Salaam ACP Jumanne Muliro amewataja Watuhumiwa hao kuwa ni OMARY ALLY, miaka 28, Mkazi wa Tegeta na mwenzake JUMA SULLEIMAN, Miaka 30, Mrangi, mkazi wa Wazo na wanunuzi wa vifaa hivyo ni AMOS JOHN, miaka 30, mkazi wa Tegeta na MOKOLO MACHAGE, miaka 26, mkazi wa Bunju.
Kamanda Muliro amesema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa April 10, 2022 na baada ya kuhojiwa wamekiri kuhusika katika matukio ya namna hiyo.
Ameongeza kuwa baada ya kupekuliwa maeneo yao walikutwa na viroba vinne vya Nyaya za Copper zilizochunwa.
Aidha Kamanda Muliro ametoa onyo kali na kuwa Jeshi la Polisi halitamvumilia mtu au kikundi chochote kinachojihusisha kwa namna yoyote ile kujaribu kuharibu miundombinu ambayo imejengwa kwa manufaa ya umma na atakayejaribu atakamatwa na mifumo ya kumfikisha kwenye vyombo vya sheria itazingatiwa.
Kamanda Muliro amesema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa April 10, 2022 na baada ya kuhojiwa wamekiri kuhusika katika matukio ya namna hiyo.
Ameongeza kuwa baada ya kupekuliwa maeneo yao walikutwa na viroba vinne vya Nyaya za Copper zilizochunwa.
Aidha Kamanda Muliro ametoa onyo kali na kuwa Jeshi la Polisi halitamvumilia mtu au kikundi chochote kinachojihusisha kwa namna yoyote ile kujaribu kuharibu miundombinu ambayo imejengwa kwa manufaa ya umma na atakayejaribu atakamatwa na mifumo ya kumfikisha kwenye vyombo vya sheria itazingatiwa.