Breaking

Sunday 22 May 2022

VISA VYA UGONJWA WA HOMA YA NYANI VYAONGEZEKA, WHO KUTOA MWONGOZO



Na Said Muhibu,Lango la habari

Ofisa wa shirika la afya ulimwenguni WHO na mtaalamu wa magonjwa ya kuambukiza David Heymann amesema kuwa ugonjwa wa homa ya nyani unaenea kwa kasi sana ulimwenguni kama magonjwa ya zinaa.

kauli hiyo ameitoa hii leo Mei 22, 2022 kutokana na ugonjwa huo kuenezwa kwa mgusano wa karibu na hivyo kuwapata watu wengi ulimwenguni tangu kuripotiwa kwa ugonjwa huo.

"Kinachoonekana kutokea sasa ni kwamba imeingia katika idadi ya watu kama njia ya ngono, katika mfumo wa uzazi, na inaenezwa kama magonjwa ya zinaa, ambayo yameongeza maambukizi yake duniani kote," David Heymann alisema.

Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa lilisema, kufikia Jumamosi, kesi 92 zilizothibitishwa na kesi 28 zinazoshukiwa za ugonjwa wa homa ya nyani, ziliripotiwa kutoka nchi 12 ikiwemo; Uingereza, Hispania na Marekani. Shirika hilo liliongeza kuwa, litatoa mwongozo na mapendekezo zaidi katika siku zijazo kwa nchi mbalimbali juu ya kukabiliana na ugonjwa huo.

Homa ya nyani ni ugonjwa wa kuambukiza ambao unapatikana sehemu za Afrika Magharibi na Kati.

Ingawa ni ya familia ya virusi sawa na ndui, dalili zake ni kali zaidi. Kwa kawaida watu hupona ndani ya wiki mbili hadi nne bila kuhitaji kulazwa hospitalini, lakini maradhi hayo huwa hatari.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages