Breaking

Sunday 13 November 2022

AJALI YA LORI NA BASI YAUA WATU 6, YAJERUHI 22 - DODOMA



Watu Sita wamefariki dunia na wengine 22 wakijeruhiwa katika ajali iliyohusisha basi la Arusha Express lenye usajili wa namba T 530 AGG kugongana uso kwa uso na lori Mchanga kampuni ya SINO-HYDRO lenye namba T 939 DZE.

Ajali hiyo imetokea leo Jumapili Novemba 13, 2022 mchana eneo la Veyula Kata ya Makutupora mkoani Dodoma.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule amesema waliofariki wote ni wanaume huku Majeruhi 10 wakiwa ni Wanawake na 12 ni Wanaume.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages