Breaking

Wednesday 5 July 2023

PURA YAWAKOSHA WANANCHI NA TEKNOLOJIA YA UHALISIA TEPE

Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imenogesha maonesho ya Saba Saba 2023 kwa kuja na kifaa maalumu kinachoonesha uhalisia tepe (virtual reality) wa namna mradi wa kusindika gesi asilia (Liquefied Natural Gas - LNG) utakavyokuwa. 

Mradi wa LNG unalenga kuendeleza gesi asilia iliyogundulika katika kina kirefu cha bahari na mitambo ya kuchakata na kusindika gesi hiyo itajengwa katika eneo la Likong'o Mkoani Lindi.

Baadhi ya wananchi waliotumia kifaa hicho wameeleza kufurahishwa na ubunifu uliotumika na kuipongeza PURA kwa kuwaletea mradi huo katika uhalisia kwa kuwa imewafanya wauelewe zaidi, tofauti na kutoa maelezo bila kuona uhalisia tepe.




Mmoja wa wananchi aliyetembelea banda la PURA akitumia kifaa cha uhalisia tepe kuangalia namna mradi wa LNG utakavyokuwa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages