Breaking

Wednesday 5 July 2023

MADINI YACHANGIA ASILIMIA 56 MAUZO BIDHAA NJE YA NCHI



Dar Es Salaam

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Madini Msafiri Mbibo, amesema kuwa mchango wa Sekta ya Madini katika kuliingizia Taifa fedha za kigeni umekuwa ukiimarika ambapo kwa mwaka 2022 Sekta ya Madini imechangia asilimia 56 ya mauzo yote ya bidhaa zilizouzwa nje ya nchi.

Hayo yameelezwa na Naibu Katibu Mkuu Mbibo leo Julai 5, 2023 alipotembelea wadau mbalimbali wa madini katika banda la Wizara ya Madini katika Maonesho ya Kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

Aidha, amewataka wadau kuzitumia taasisi zilizo chini ya wizara Tume ya Madini, Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) na Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) ili Sekta ya Madini iweze kuchangia zaidi katika Pato la Taifa.

Katika hatua nyingine, Mbibo amezungumza na wadau wa Sekta ya Madini waliopo katika banda hilo ambao wamemweleza huduma wadau wanazotoa, fursa zilizopo katika maeneo ya shughuli zao.

Naibu Katibu Mkuu Mbibo aliongozana na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) Dkt. Mussa Budeba na wadau wengine wa Sekta ya Madini.











Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages