Breaking

Thursday 3 August 2023

DKT. BITEKO ATETA NA KAMPUNI YA SOTTA MINING DODOMA



Waziri wa Madini Dkt. Doto Biteko leo Agosti 3, 2023 jijini Dodoma amekutana na Uongozi wa Juu wa Kampuni ya Sotta Minerals Corporation Limited ambayo ni ya ubia Kati ya Serikali na kampuni ya Orecorp Tanzania limited ya Australia inayosimamia Mradi wa uchimbaji madini ya dhahabu uliopo wilayani Sengerema Mkoani Mwanza.

Kupitia Mkutano huo, kampuni ya Sotta imeeleza maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo ambao unatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwaka 2025.

Aidha, Dkt. Biteko ameelezwa kuwa, hivi sasa kampuni iko kwenye hatua za mwisho za kuweza kuwalipa fidia wananchi walio ndani ya eneo la mradi ili kuwezesha mradi huo kuanza.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages