Breaking

Wednesday 4 October 2023

TBS YATOA ELIMU KWA WAJASIRIAMALI KWENYE MAONESHO YA TIMEXPO

SHIRIKA la Viwango Tanzania TBS wametoa elimu kwa wazalishaji wa Bidhaa za Viwandani na wajasiriamali juu ya dhana ya ubora wa bidhaa katika Maonesho ya Kimataifa ya Viwanda Tanzania 2023 (Times Expo 2023)

Akizungumza katika Maonesho hayo leo Oct 4,2023 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa TBS,Dkt. Athuman Ngenya amesema maonesho haya yanakutanisha wenye Viwanda Tanzania, Wajasiriamali na watu wengine wanaokwenda kumtembelea maonesho hayo hivyo shughuli yao kubwa ni kuhakikisha Wana elimisha wazalishaji kuzalisha bidhaa bora.

"Bidhaa zikiwa na ubora zinakua na faida nyingi,moja nikujiamini lakini pia zinakuwa na soko kubwa itauzika ndani ya nchi na nje ya nchini". Amesema

Ameeleza kuwa lengo la TBS ni kuhakisha inawafikia wajasiriamali na watuamiaji wa mwisho wa bidhaa kuzitambua na kuchagua bidhaa Bora ili wapate kulingana na thamani ya pesa yao.

Pamoja na hayo ametoa wito kwa wazalishaji wa Bidhaa ambazo hazina nembo ya TBS wakajisajiri TBS ili kupata alama ya ubora na amewasihi wananchi kukagua bidhaa wanazo nunua kama zina alama ya ubora kwa ajili ya usalama wao na thamani ya fedha kulingana na ubora.

"Kisheria kiwanda chochote kinachozalisha bidhaa yeyote ambayo haijapitia TBS ni makosa"amesema

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages