Breaking

Sunday 5 November 2023

BANDARI QUEENS BINGWA NETIBOLI DARAJA LA PILI, MENEJIMENTI YA TPA YAPONGEZWA

Timu ya Netiboli ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania- TPA “ Bandari Queens” imetwaa Ubingwa wa Mashindano ya ligi Daraja la pili Taifa baada ya kupata ushindi wa magoli 38 kwa 31 dhidi ya Mapinduzi Dodoma Katika mchezo wa tamati uliochezwa Uwanja wa Shule ya Sekondari Nsimbo, Mpanda Mkoani Rukwa.

Mkuu wa wilaya ya Mpanda Mhe. Jamila Yusuph amekabidhi kombe kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages