Breaking

Tuesday 30 January 2024

UDSM YAJA NA VIPAUMBELE KUIMARISHA TAFITI NCHINI KUFIKIA VIWANGO VYA KIMATAIFA

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

CHUO Kikuu cha Dar es Salaam, Ndaki ya Sayansi za Jamii wameadhimia kufikisha Tafiti zinazofanyika kusikika na kuchapishwa katika majarida ya Kimataifa kwa kuboresha machapisho na kuongeza nguvu katika majarida ya ndani kwa lengo la kuwa na maendeleo endelevu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 30,2024 katika kikao kujadili utafiti kuhusu machapisho na kitaaluma katika Vyuo- Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, Rasi wa Ndaki ya Sayansi za Jamii Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Christine Noe amesema ni vizuri kuzipatia thamani tafiti zinazofanywa nchini,kwa kuweka mazingira ya kuzipandisha katika viwango vya kimataifa katika majarida ya ndani.

"Kila kitu unachokiona cha kimataifa kimeanzia katika mataifa fulani, kwahiyo na sisi tunachojifunza kikubwa ni vizuri kukipa thamani ya Kimataifa vitu na tafiti, kama tutaboresha machapisho yetu na tukipandisha majarida yetu kimataifa italeta sifa kwa nchi". Amesema Prof. Noe.

Aidha Prof. Noe ameeleza kuwa majarida ya ndani yasipopewa nguvu nchi itapoteza kitu kikubwa na kukosea kuwa na maendeleo endelevu katika tafiti zinazofanywa.

"Tunashukuru wenzetu wamefanya tafiti na takwimu ya ile michakato kwahiyo tunaendelea kujadiri mambo haya maana ndio yanayo Jenga hata ile mijadara ya kitaifa "Prof. Noe ameeleza.

Pamoja na hayo amesema kuhusiana na changamoto ambazo wanakumbana nazo katika tafiti kufikia katika majarida makubwa ya nje ambapo imebua bidii ya kuandaa taarifa za tafiti zinazofanywa katika viwango vikubwa.

Kwa Upande wake Mtafiti kutoka Chuo Kikuu Cha Autonoma Barcelona-Prof. Dan Brockington amesema kuwa katika tafiti za kimataifa mafanikio makubwa yanapatikana kwa kushirikiana na mataifa mengine kwa kuongeza elimu na kutoa matokeo kwa pamoja ili kuinua ujuzi kwa watu wote.

Aidha ameeleza kuwa tafiti za nchini zimetawaliwa na ukimya mkubwa kwa sababu haziifikii jamii ya ulimwengu ingawa zipo katika viwango vya kimataifa ambapo amesema kasoro nijambo ambalo lipo katika tafiti nyingi ulimwenguni na jambo la msingi ni kutatua changamoto hizo.

Naye Mhadhiri Idara ya Sosholojia na Anthropolojia Kikuu Cha Dar es Salaam- Bw. Egidius Kamanyi amesema kuwa wamefahamu mapungufu ya machapisho yaliyokuwa yamechapishwa ambapo italeta mageuzi ya kukuza majarida ya ndani na kukuza katika viwango vya tafiti.
Mtafiti kutoka Chuo Kikuu Cha Autonoma Barcelona-Prof. Dan Brockington akizungumza katika kikao kujadili utafiti kuhusu machapisho na kitaaluma katika Vyuo- Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam kilichofanyika leo Januari 30, 2024 UDSM Jijini Dar es Salaam
Mtafiti kutoka Chuo Kikuu Cha Autonoma Barcelona-Prof. Dan Brockington akizungumza katika kikao kujadili utafiti kuhusu machapisho na kitaaluma katika Vyuo- Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam kilichofanyika leo Januari 30, 2024 UDSM Jijini Dar es Salaam
Mtafiti kutoka Chuo Kikuu Cha Autonoma Barcelona-Prof. Dan Brockington akizungumza katika kikao kujadili utafiti kuhusu machapisho na kitaaluma katika Vyuo- Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam kilichofanyika leo Januari 30, 2024 UDSM Jijini Dar es Salaam
Mtafiti kutoka Chuo Kikuu Cha Autonoma Barcelona-Prof. Dan Brockington akisisitiza jambo wakati akizungumza katika kikao kujadili utafiti kuhusu machapisho na kitaaluma katika Vyuo- Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam kilichofanyika leo Januari 30, 2024 UDSM Jijini Dar es Salaam
Rasi wa Ndaki ya Sayansi za Jamii Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Christine Noe akizungumza katika kikao kujadili utafiti kuhusu machapisho na kitaaluma katika Vyuo- Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam kilichofanyika leo Januari 30, 2024 UDSM Jijini Dar es Salaam
Mhadhiri Idara ya Sosholojia na Anthropolojia Kikuu Cha Dar es Salaam- Bw. Egidius Kamanyi akizungumza katika kikao kujadili utafiti kuhusu machapisho na kitaaluma katika Vyuo- Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam kilichofanyika leo Januari 30, 2024 UDSM Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages