Breaking

Wednesday 15 May 2024

BAISKELI YA MAMA IMEFIKA SAME

Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao (MOM) imeendelea kupokea maombi mengi kutoka kila pande ya Tanzania kutoka kwa ndugu zetu wenye uhitaji wa Baiskeli hizi.

Kama Taasisi, tunapenda kutoa shukran zetu za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wasanii na Wadau mbalimbali wapenda maendeleo kwa kuhakikisha kwamba Taasisi inatimiza kile tulichoagizwa na kuelekezwa kufanya.


"Na leo hii, Baiskeli hii ya Mama imefika Wilayani Same, na tuna nia ya dhati kuhakikisha tunasaidia ndugu zetu wengi zaidi wenye uhitaji'',alisema Mwenyekiti wa Taasisi hiyo almaarufu Steve Nyerere.





Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: +255 621 896 990

Pages