Breaking

Thursday 20 October 2022

MUME ADAIWA KUMUUA MKEWE, MWILI AUFUNIKA MIFUKO YA SARUJI NA KUUTUPA




Mkazi wa Kata ya Bahi Sokoni, Juma Linoga anadaiwa kumuua mkewe, Mariam Alex (34) kisha mwili wake kuufunika na mifuko ya saruji ndani ya pagale.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno alisema jana kuwa mauaji hayo yalitokea Oktoba 15 mwaka huu na mtuhumiwa wa tukio hilo amekimbia.

Alisema mwili wa Mariam uligundulika katika pagale hilo saa 9.30 alasiri baada ya taarifa kutolewa.

“Tuliukuta mwili ukiwa umepigwa na kitu sehemu mbalimbali lakini bado tunafanya uchunguzi kujua chanzo cha mauaji hayo ni nini ili hatua kali zichukuliwe kwa waliohusika,” alisema Otieno.

Kamanda Otieno alisema baada ya mauaji hayo, mtuhumiwa alikimbia na jeshi hilo linaendelea kumtafuta ili ahojiwe.

Soma zaidi >>HAPA<<

Via - Mwanachi 


Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages