Breaking

Tuesday 29 November 2022

AJALI YAUA WATATU, YAJERUHI MMOJA SINGIDA



Watu watatu wamefariki dunia baada ya kupata ajali katika Kijiji cha Kitopeni Halmashauri ya Itigi wilayani Manyoni mkoani Singida, huku mmoja akipatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa ya Mtakatifu Gaspar Itigi.

RPC Singida Stella Mutabihirwa, amesema ajali hiyo imetokea usiku wa kuamkia Novemba 27, 2022 na ilihusisha lori na gari ndogo aina ya Mazda.

"Ajali hiyo ilisababisha vifo vya watu wawili papo hapo, na mmoja alifariki wakati anapatiwa matibabu, chanzo cha ajali ni uzembe wa dereva wa lori ambaye alihama kabisa upande wak na kulifuata gari dogo na kusababisha ajali hiyo," amesema ACP Mutabihirwa




Via: EATV
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages