Breaking

Tuesday 29 November 2022

WANANCHI KENYA WALIA NA UHABA WA CONDOM



Wasiwasi unashuhudiwa katika Kaunti ya Bungoma kufuatia uhaba wa mipira ya ngono - uhaba ambao umekumba kaunti hiyo ya ukanda wa Magharibi kwa miezi kadhaa sasa.

Uhaba huu umechangia pakubwa ongezeko la visa vya maambukizi vya ukimwi pamoja na mimba za mapema miongoni mwa vijana wa kaunti hiyo.

Afisa wa Kuthibiti Ukimwi katika Kaunti ya Bungoma Fred Barasa anasema kuwa hali ni mbaya, vijana wengi wakikosa kujikinga dhidi ya magonjwa ya zinaa kama vile ukimwi.

Kwa mujibu wa Barasa, wanawake ambao hawawezi kumudu gharama ya mipira mipya ya ngono wameamua kuosha iliyotumika na kuitumia kwa mara nyingine - hili likuwa hatari.

Wakaazi wanasema kuwa uhaba huu hususan msimu huu wa sherehe za Disemba utaharibu mambo kabisa eneo hilo kwa mimba za mapema na maambukizi ya magonjwa.

Wakaazi sasa wanatoa wito kwa serikali kuhakikisha mipira ya ngono inafika katika Kaunti ya Bungoma wakidai kuwa maisha yao kako hatarani.

Tatizo la kondomu Bungoma na Kenya nzima Mipira ya ngono ya bwerere hupewa kama msaada kutoka kwa hazina ya dunia.

Kwa mujibu wa ripoti, Kenya inakabiliwa na uhaba wa milioni 50 za mipira ya ngono - raia ambao hulengwa na mipira hii wakiathirika pakubwa.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages