Breaking

Monday 28 November 2022

WATU WATATU WATUHUMIWA KUMUUA BODABODA NA KUNYOFOA VIUNGO VYAKE




Watatu wakazi wa Kiteto mkoani Manyara akiwemo mwalimu wa sekondari Lesoiti, wamefikishwa katika Mahakama ya wilaya ya Kiteto, kwa tuhuma za kumuua dereva bodaboda na kunyofoa baadhi ya viungo vyake kwa imani za kishirikina.

Watuhumiwa hao wamefikishwa mahakamani leo Novemba 28, 2022, baada ya jitihada ya Jeshi la Polisi Kiteto kufuatilia mawasiliano yao toka awali kabla ya mauaji hayo.

Watuhumiwa hao wanadaiwa kutenda kosa hilo Oktoba 21, 2022, ambapo baada ya kutekeleza mauaji yao walinyofoa viungo hivyo vya mwili wake.

Shtaka hilo limetajwa na watuhumiwa hawakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina uezo wa kusikiliza kesi hiyo na kesi imeahirishwa hadi Desemba 12, 2022.


Via: EATV
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages