Breaking

Tuesday 20 December 2022

RADI YAUA MMOJA - NJOMBE



Calista Haule (15) mkazi wa kijiji cha Lifua kata ya Luilo wilayani Ludewa mkoani Njombe amefariki baada ya kupigwa na radi wakati akiwafunga mbuzi chini ya mti baada ya kuwatoa malishoni.



Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo wamesema binti huyo alipigwa na radi hiyo na kufa papo hapo sambamba na mbuzi aliokuwa akiwafunga

Baba wa binti huyo pamoja na dada yake wameelezea masikitiko yao na kudai kuwa binti huyo alirejea nyumbani wiki moja iliyopita akitokea shuleni Mafinga mkoani Iringa kwa ajili ya likizo baada ya shule kufungwa.

Via: EATV
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages