Breaking

Monday 16 January 2023

RAIS DKT. MWINYI ATEUA KAMISHNA MKUU ZRA



RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt.Hussein Ali Mwinyi amemteua ndugu Yusuph Juma Mwenda kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA).

Kupitia taarifa iliyotolewa leo Januari 16, 2023 na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar, Mhandisi Zena A.Said imeeleza kuwa uteuzi huo umeanza Januari 10, 2023.

"Kufuatia kufutwa kwa Sheria ya Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) ya mwaka 1996 na kutungwa Sheria ya Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA) ya mwaka 2022.

"Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt.Hussein Ali Mwinyi amemteua ndugu Yusuph Juma Mwenda kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA),"imeeleza taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, ndugu Yusuph Juma Mwenda alikuwa Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB).


Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages