Breaking

Monday 29 May 2023

ALIYOYASEMA DC JOKATE BAADA YA KUFANYIKA MAMATHON KOROGWE


Na Mwandishi Wetu Korogwe

MKUU wa Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga Jokate Mwegelo amesema kuwa kazi kubwa inayofanywa na Serikali katika kuboresha miundombinu za huduma mbalimbali ya afya lengo lake ni kumsogea huduma karibu na mwananchi.

Jokate ametoa kauli hiyo baada ya kufanyika kwa mbio ambazo zilikuwa zimeaandaliwa kwa wanawake wajawazito wilayani humo na kupewa jina la Mamathon ambapo zaidi ya wajawazito 2000 wameshiriki sambamba na kupatiwa vifaa kwa ajili ya kujifungulia.

"Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anaguswa na changamoto mbalimbali husani huduma za akina mama na watoto na wao, hivyo kupitia Mamathon tunaenzi yale mema na mazuri ambayo Rais wetu amekuwa akiyafanya kupitia Serikali yake ya Awamu ya sita kwa watanzania na zaidi kwenye kundi la akina mama na watoto."

"Sisi akina mama ndio walezi wa jamii zetu, ndio wajenzi wa Taifa kwa maana ukizungumzia watoto wanatoka tumboni mwetu ndio kwa namna moja ama nyingine na wanaume wao wamekuwa wakitusaidia katika malezi lakini kubwa zaidi , akina mama ndio wanatunza hawa watoto."

Jokate amesema Korogwe waliandaa Mamathon ni mahususi kwa ajili ya kumsemea Rais Dk.Samia Suluhu Hassan Samia ambaye ameweika mbele ajenda za mwana mama na mtoto"Kwa hiyo hili tukio sio tukio tu la kutembea lakini kubwa kwenda kuwa mabalozi wa Rais wetu kwani mwendo ameuaza vizuri ,mwendo atauendeleza na sisi wote tunatakiwa kuungana naye."

Aidha amewaeleza akina mama wajawazito kuwa Serikali ya Awamu ya Sita lengo lake nikupeleka huduma za afya kwenye maeneo yao na kwa Wilaya ya Korogwe hakuna kata ambayo haina huduma ya afya.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Pangani Zainab Abdallah na Meya wa Temeke mkoani Dar es Salaam Abdallah Mtimika wametumia nafasi hiyo kumpongeza Jokate kwa kufanya tukio la kuleta hamasa kwa wamama wajawazito kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi na kuzingatia lishe bora.

Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya ya Pangani Zainab Abdallah amesema jambo ambalo amelifanya Mkuu ws Wilaya Jokate ni kubwa na ni jambo la mama."Nimekuja hapa kwa niaba ya wakuu wa Wilaya wote Mkoa wa Tanga, tunampongeza kwani anaupiga mwingitangu ameingia wilayani Korogwe."

Amesema wananchi wa Wilaya ya Korogwe wamelamba dume na kama ni madini basi ya Tanzanite ambayo yanazalishwa Tanzania peke yake.

Amefafanua Jokate ameupiga mwingi akiwa katika Wilaya ya Kisarawe,Temeke na Meya wa Temeke ametoa ushuhuda lakini kubwa zaidi amewaeleza wananchi wa Korogwe kwamba Rais Dkt Samia Suluhu Hassan amewapendelea kwani amewapelekea jembe na sasa wanashuhudia Mamathon.

Amesema kupitia Mamathon , Jokate amefanya jambo kubwa kubwa linalowagusa maisha ya wanawake.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages