Breaking

Monday 29 May 2023

AMCHINJA MAMA YAKE BAADA YA KUNYIMWA CHAI



Mwanamume mmoja amemuua mamake kwa kumchinja baada ya kunyimwa kikombe cha chai katika kijiji cha Alupe, wilayani Busia, katika nchi jirani ya Uganda. 


Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo, Robin Barasa alimchinja mamake mwenye umri wa miaka 53 kutumia panga baada ya kunyimwa chai mnamo Jumatano asubuhi. 


Umati wa watu wenye hamaki ulishambulia Robin na kumpiga kwa mawe hadi kuaga dunia kwa kosa la kumkata shingo na kumuua Pelvine Barasa. 


Kwa mujibu wa ripoti ya kituo cha redio cha Emuria FM, mama huyo aliamua kumnyima chai mwanawe baada ya kukataa kulima shamba la mahindi. 


Babake Robin na mumwe Pelibe - Robert Ongaria alisimulia kuwa aliondoka nyumbani kwenda kazini katika Hifadhi ya Maiti ya Alupe lakini akapigiwa simu na mwenyekiti wa kijiji kuwa nyumbani kwake kulikuwa kumeharibika. 


Ghasia na mayowe yalivutia wanakijiji ambao walitembea mpaka nyumbani kwa Pelvine na kumkuta ameuawa katika shamba la mahindi. 


Kulingana na wanakijiji, Robin alimfuata mama yake nyuma ya nyumba, akamdhibiti na kumkata shingo kwa kutumia panga kabla ya kuitupa. 


Viongozi katika Jumuiya ya Alupe wamekemea tukio hilo na kuwataka vijana kuepuka matumizi ya dawa za kulevya. 


Maiti za wanafamilia hao wawili zimepelekwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti wakati uchunguzi unafanywa na mamlaka za Uganda. 


Chanzo: Tuko News


Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia langolahabari@gmail.com au WhatsaApp: + 255 621 615 613 au +255 621 896 990

Pages